Email: info@jkuz.go.tz  |  P.o.Box: 985  |  Tel: 0242238030  |  Fax: 0242232149


Logo
HABARI NA MATUKI0

MAHAFALI YA WANAFUNZI SKULI YA SEKONDARI JKU MTONI

Created at 1 month ago

Mkuu wa JKUZ

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ndugu Ali Abdul-ghulam Hussein amezipongeza Skuli za Ufundi na Sekondari JKU Mtoni kwa jitihada za kuimarisha Sekta ya Elimu Nchini

Ameyasema  hayo  katika  Ukumbi  wa  Skuli  ya U JKU  wakati wa mahafali ya kuwapongeza  wanafunzi wa Skuli za Ufundi na Sekondari JKU Mtoni

Amesema ni jukumu la wazazi na walezi kuwekeza elimu kwa watoto wao ili waweze kupata fursa za kuendelea na elimu ya juu sambamba na kupata nafasi za kimasomo ndani na nje ya Nchi ili kuweza kujikwamua katika maisha yao ya badae

Hata hivyo ameahidi kuwapatia walimu wa Skuli ya Sekondari vishkwambi  kwa lengo la kuwaongezea uwezo  sambamba  na kuendana na wakati katika ufundishaji

Nae Mkuu wa JKU Kanali Makame Abadalla Daima amesema mafanikio ya Skuli za Ufundi na Sekondari JKU Mtoni yanatokana na mashirikiano baina ya wazazi, wanafunzi pamoja na jitihada  zinazofanywa na walimu hasa katika kudumisha nidhamu katika kipindi chote cha masomo

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Skuli za Ufundi na Sekondari Kanali Jabir Saleh Simba amesema jumla wanafunzi  234  wamefanya mitihani ya kidatu cha nne na wote wamefanikiwa kufaulu katika daraja la kwanza la pili na la tatu jambo ambalo limeiyongezea sifa Skuli ya JKU

Akisoma  taarifa kwa niaba ya wanafunzi wenzake Talatham Abadalla Mussa amesema licha ya ufaulu mzuri uliopatikana likini kuna changamoto ndogo ndogo kama vile ukosefu wa usafiri pamoja na dahalia ambalo lingesaidia wanafunzi katika jitihada za masomo

JKU YAFANYA KAZI USIKU NA MCHANA KATIKA UJENZI WA MRADI WA SOKO LA MWANAKWEREKWE

MKUU WA WILAYA YA MJINI AKABIDHIWA MRADI WA MAJENGO YA WAJASIRIAMALI NA JESHI LA KUJENGA UCHUMI


WASILIANA NASI
  • Email: info@jkuz.go.tz
  • P.O.Box: 985
  • Fax: 0242232149
  • Tel: 0242238030
WALIOTEMBELEA TOVUTI