Email: info@jkuz.go.tz  |  P.o.Box: 985  |  Tel: 0242238030  |  Fax: 0242232149


Logo
HABARI NA MATUKI0

UFUNGAJI WA MAFUNZO YA UNGOZI WA KATI

Created at 4 months ago

Mkuu wa JKUZ

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Uchumi JKU Kanali Makame Abdalla Daima aliwataka wahitimu wa kozi ya  Uongozi  wa kati  kuyatumia  vyema mafunzo  waliyopata  kwa lengo  la kuongeza ufanisi ndani ya jeshi hilo.

  Aliyasema  hayo  wakati  akifunga  mafunzo  ya kozi  ya uongozi  wa kati  mkupuo  wa  08 \2022  iliyofanyika  katika  Chuo  cha  uongozi  JKU  Dunga   Wilaya ya Kati Unguja .

Alisema kuwa  madhumuni  makuu  ya mafunzo hayo  ya kijeshi  ni kuwajengea  uwezo  wa  kiutendaji  watumishi  wa  JKU sambamba  na  kuongeza  ufanisi  katika  utekelezaji  wa majukumu  yao  ya kila siku

Hata hiyo  alieleza  kuwa  nidhamu , uwajibikaji  na ushirikiano  katika  kazi ndio njia  pekee itakayosaidia  kuongeza uzalishaji  katika  kambi  mbalimbali za JKU.

Akisoma taarifa ya mkufunzi  mkuu  wa kozi  hiyo  Luteni  Idi  Haji  Makame  alisema kuwa jumla  ya  wanafunzi  427  wamefanikiwa  kuhitimu  mafunzo  ya  miezi   minne [4] katika  masomo  mbalimbali   ya kijeshi  kama vile Ujanja wa porini Usomaji wa ramani, Mbinu za kuvita pamojana uzalendo wanchi yao .

Akisoma  taarifa  kwa niaba  ya  wahitimu  wenzake  mteule  daraja la pili  Nasra  Abdala  Makolela  alisema  kuwa licha  ya  mafanikio  waliyoyapata  lakini  pia  kuna changamoto  zinazowakabili ikiwa ni pamoja   na udongo wa kituo cha afya  na  ukosefu  wa vifaa tiba, ukosefu wa maktaba ya kijeshi  pamoja  na uchakavu  wa  miundombinu ya barabara .

Hata hivyo  alieleza kuwa  pamoja  kushiriki  kikamilifu  katika  mafunzo  hayo  pia walishiriki  katika  majukumu  mbali mbali  ya  Kitaifa  kama  vile   zoezi  la  Linda  Kisiwa namba mbili ( 2 )  pamoja  na kushiriki katika  Sensa  ya Watu  na  Makaazi

Alisema  mbali na  mafunzo  hayo  lakini  pia wamefanikiwa   kuchangia  jumla  ya  shilingi  milioni  arubaini  na sita laki tisa na elfu sabiini  ambazo  zitasaidia   katika  ujenzi wa ofisi , vyoo, pamoja na mnara wa maji  ili kuweka alama  ndani ya chuo hicho .

Sherehe hizo ziliambatana  na utoaji wa vyeti na zawadi kwa wanafunzi walofanya vizuri pomoja na maonyesho  ya  harusi za kijeshi ,  kwata ya kitara   pamoja na kwata  ya kutawanya mikusanyiko haramu.

JKU YAFANYA KAZI USIKU NA MCHANA KATIKA UJENZI WA MRADI WA SOKO LA MWANAKWEREKWE

MKUU WA WILAYA YA MJINI AKABIDHIWA MRADI WA MAJENGO YA WAJASIRIAMALI NA JESHI LA KUJENGA UCHUMI


WASILIANA NASI
  • Email: info@jkuz.go.tz
  • P.O.Box: 985
  • Fax: 0242232149
  • Tel: 0242238030
WALIOTEMBELEA TOVUTI